Safaree afuta tattoo za Nicki Minaj



Imeshindwa kueleweka haraka kama ni hasira, wivu au ni kweli amesahau kabisa mapenzi ya Nicki Minaj?. 

Huyu si mwingine bali ni Safaree ambaye alikuwa Boyfriend wa female rapa Nicki Minaj.
Safaree ametupia picha kwenye instagram yake ambayo ameonyesha kufuta tattoo za Nicki Minaj moja ni ile iliyo kuwa kwenye mkono wake wa kulia, na ile iliyokuwa kwenye upande mmoja wa kifua chake.
tatoo 2
Muonekano wa tattoo mpya mkononi mwa Safaree

Safaree amefuta tattoo hizo ambazo haikutegemewa kwamba ingefutika maishani kwani ilichorwa kwa ubora wa hali ya juu lakini hatimaye tattoo zimefutwa na kuchorwa tattoo nyingine ya ua juu yake.

“Unafikiri ingekuwa ngumu?…nimefanikiwa, sorry NickiMinaj” hayo ni maelezo “caption” ya picha hiyo ya tattoo mpya mkononi yaliyo andikwa na Safaree.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment