Abby Skillz Hatopotea Tena kwenye Game Amerudi ndio Karudi Moja kwa Moja kama Gari limewashwa halizimwi Tena.

Unaikumbuka Ngoma kama Ngo ngo,Nakupenda ambazo zilifanya vizuri sana na tunakumbuka aliwapa support washikaji  zake Alikiba na Mr Blue na Sasa amerudi na ngoma mpya inaitwa Averina ambayo imekuwa Gumzo kitaa wadau walimmiss sana mshikaji baada ya kupotea kwa muda kidogo.

Akizungumza na Vmix ya channel ten Abby amesema majukumu ya kimaisha yalimfanya awe kimya kidogo kwa muda licha ya kuachia ngoma kwa kipindi cha hivi karibuni lakini hazikufanya poa,Na Averila ni ngoma ambayo mwaka mmoja uliopita ilianza kutengenezwa na Nje ya Averina amesema kuwa kuna ngoma nyingine ambazo wameshazifanya wanasubiri kuziachia tu,

Amesema kuwa kunaproject kubwa ambayo wameifanya ikisimamiwa na Yeye mwenyewe ,Mr blue pamoja na Alikiba ilikufanikisha mziki wa Bongoflava kufika mbali na watu waamini kuwa amerudi vizuri katika game na kwa namna ya kipekee.

Baada ya kuulizwa na Mtangazaji wa kipindi hicho Mwaka Ze Bwoy  kuhusu kama Alikiba na Mr Blue nje ya mchango wa kimawazo wanaoutoa Je Kuna kiasi cha fedha chochote wanachokitoa Abby amesema kuwa ieleweke kuwa kila kitu wanakisimamia pia na wanamchango mkubwa katika hiyo project.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment