Azealia Banks: Hip hop inadhalilisha wanawake weusi, haieshimu jinsia ya kike.


‘Female’ rapper Azealia Banks, amelalamikia viombo vya habari vinavyomilikiwa na wamerekani weusi pamoja na mziki wa Hip Hop kuwa wamekuwa sehemu ya kudhalilisha wanawake.

Banks ametumia ‘time’ kuandika Tweet zaidi ya 18, akifafanua jambo hilo zaidi akidai ‘black media’ Marekani ndio zimechangia kuua ‘brand’ na mziki wake.

“Black man wanaruhusiwa kubaka, kuua watu, kufanya mapenzi na watoto wadogo na bado wanasifiwa na kuungwa mkono na muziki wa Hip Hop kama jambo la sifa.

Black Media wamechangia vikubwa kupoteza ‘brand’ yangu, wakati nmeathiriwa kisaikolojia na TI wote mlinicheka, nawataka kutotumia vituo vyenu kupiga nyimbo zangu nimechoka na nyie” ameandika Azealia Banks.

Katika ‘Tweet’ zingine, Azealia Banks amevitaka vituo vya ‘radio’ na ‘tv’ vinavyomilikiwa na weusi kama BET, Hot 97, Power fm, Hip hop DX, Power wave na vingine vingi kutokucheza mziki wake wale kuongelea na kuandika chochote kuhusu yeye.
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment