Baba abaka Watoto Wake


Ajiboye Oluwaseyi (37), Mkazi wa mji wa Ondo huko nchini Nigeria amekamatwa na Polisi na kutupwa ndani baada ya kushtakiwa kwa kosa la ubakaji kwa watoto wake.

Kwa mujibu wa Mama wa watoto hao, amesema yeye na mume wake waliachana tangu mwishoni mwa mwaka jana 2014, hivyo mume wake aliamua kuondoka na watoto hao ambao wawili ni watoto wake mwenyewe na mmoja ni mtoto wa baba mwinginge yani mtoto wake wa kambo.

Msemaji wa Polisi wa mji wa Logos DSP Patricia Amadin, amethibitisha kukamatwa kwa Baba wa watoto hao, ambao mmoja ana miaka 4, mwingine 6 na mtoto wake wa kambo ana miaka 15.
Vipimo kutoka kituo cha afya vimetoa ripoti yake ambapo imethibitisha kwamba ni kweli watoto hao walifanyiwa kitendo hicho cha kinyama mara kadhaa.

Mama wa watoto hao alipewa taarifa na majirani kwamba huenda mzazi mwenzake alikuwa anawabaka watoto wake kwani mwenendo wake ulikuwa haueleweki ambapo muda mwingi alikuwa akijifungia ndani na watoto wake.

Mama alipata nafasi ya kuongea na moja kati ya mtoto wake ambapo alimwambia ukweli kwamba Baba yao alikuwa anawafanyia kitendo hicho, ndipo hapo Mama huyo alipokwenda kustaki polisi.
Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa na huenda Baba huyo akakumbana na adhabu ya kifungo cha maisha gerezani.

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment